Ufunuo Aliopewa kwa Yohane

Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi, na kutoka kwa-Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia.

Salamu kwa makanisa saba

Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu, akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina.

Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.

"Mimi ni Alfa na Omega," asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.

Kwa malaika wa kanisa la Laodikea andika hivi:

Tarumbeta

Kisha wale malaika saba wenye tarumbeta saba wakajiweka tayari kupiga mbiu ya mgambo. ic

Malaika...

Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake. Mchanganyiko wa mvua ya mawe na moto, pamoja na damu, ukamwagwa juu ya nchi. Theluthi moja ya nchi ikaungua, theluthi moja ya Miti ikaungua, na majani yote mabichi yakaungua.
Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake.
Na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto ukatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikawa damu, theluthi moja ya viumbe vya baharini vikafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
Kisha malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake.
Na nyota kubwa ikiwaka kama bonge la moto, ikaanguka kutoka mbinguni, na kutua juu ya theluthi moja ya mito na chemchemi za maji.
Nyota hiyo inaitwa "Uchungu."
Basi, theluthi moja ya maji yakawa machungu; watu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.
Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta yake.
Ndipo theluthi moja ya jua, ya mwezi na ya nyota ikapata pigo; hata mwangaza ukapoteza theluthi moja ya mng'ao wake. Theluthi moja ya mchana ikakosa mwanga, hali kadhalika na theluthi moja ya usiku.
Kisha nikatazama, nikasikia tai akiruka juu kabisa angani anasema kwa sauti kubwa, "Ole, ole, ole kwa wanaoishi duniani wakati malaika watatu waliobaki watakapopiga tarumbeta zao!"
Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu.

Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu. Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.

Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti oyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.

Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano.

Maumivu?

Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
  1. Muda huo watu watatafuta kifo
    1. lakini hawatakipata;
    2. watatamani kufa
    3. lakini kifo kitawakimbia.
  2. Kwa kuonekana, nzige
    1. hao walikuwa
    2. kama farasi waliowekwa
    3. tayari
  3. Kwa vita.
    1. Juu ya vichwa vyao walikuwa
      1. na taji zilizo kama za
      2. dhahabu, na
        1. hao walikuwa
        2. kama farasi waliowekwa
        3. tayari
      3. nyuso zao zilikuwa
    2. kama za binadamu.

Nywele zao...

Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.

Vifua vyao...

Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.

Walikuwa na mikia...

Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano. Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi.
Sean M. Burke, 1 May 1995